Advertisement
Umenifuta alama ya upendo Kwenye penzi langu Tena ukashindwa kuficha matendo Kwenye mboni langu
Najihisi moyo una ganzi Ngumu kufika safari yangu Kinywa kibogoyo silambi Wala kutafuna
Aliniteka akili yangu Nikazama mazima mazima Mwisho wa siku ikala kwangu Kichwa ikabaki na jina
Oooh yanauma Ndio maana kila siku shida shida Tajiri wa huzuni Ndonda limekosa tiba Nitapona lini?
Mie eh acha iwe, we acha iwe Acha iwe, bora nibaki mwenyewe Acha iwe, we acha iwe Acha iwe, bora nibaki mwenyewe
Advertisement
Nilishapona kidonda Ona kaja kukitonesha Kinywa nong’ona kupenda Nakosa jibu kuwtwa nakesha
Naumwa kuwaza eh Huenda pengine moyo hujaridhia Nyota angaza eh Mizani nipime wapi nafsi itatulia
Ama ni nuksi mikosi Nyota ya punda yangu kubeba mizigo Ninakazana kufosi Cha jana kuvunda kwangu mi nishazoe
Kila siku shida shida Tajiri wa huzuni Ndonda limekosa tiba Nitapona lini?
Mie eh acha iwe, we acha iwe Acha iwe, bora nibaki mwenyewe Acha iwe, we acha iwe Acha iwe, bora nibaki mwenyewe
Kila siku shida shida Tajiri wa huzuni Ndonda limekosa tiba Nitapona lini mie